KOZI ZA UKOCHA ZISAIDIE KULETA MAPINDUZI KATIKA SOKA
LIPULI FC IRUDI NA MOTO WA ZAMANI LIGI KUU
YANGA TULIENI VINGINEVYO MTAZIDI KUPOTEA
TUCHAGUE VIONGOZI BORA ILI TUPIGE HATUA MICHEZONI
SIMBA, YANGA ACHENI MAMBO YA KIZAMANI
'KIKI NI UFINYU WA MAWAZO'
TIMU ZA LIGI KUU ZIWEKEZE ZAIDI KATIKA TIMU ZA VIJANA
WASANII, WANAMICHEZO WATHAMINIWE
SIMBA NA YANGA ZINAONGOZA KWA KUUA VIPAJI VYA WACHEZAJI NCHINI
KUTOFANYIKA TAIFA CUP KUMEUA HAMASA YA SOKA MIKOANI
YANGA MDHARAU MWIBA.....
VILABU VIWE WAZI KATIKA USAJILI WA WACHEZAJI
SAPOTI KUBWA KWA TIMU YA TENISI KWENYE KOMBE LA DUNIA
SIMBA CHEZENI MPIRA ACHENI KULIALIA
MISS TANZANIA ZAIDI YA SHINDANO, LIMEWATOA WENGI
SINGIDA UNITED, LIPULI NA NJOMBE FC JIPANGENI MSIISHIE KUSINDIKIZA VPL
YANGA YAAJIRI VIONGOZI WAPYA 4
KLABU ya Yanga imeajiri maofisa wanne wapya,ambao ni Khamis Jecha,Jimmy Kindoki ( Idara ya Wanachama na Mashabiki),Willy Shemoka (Idara ya Habari na Mawasiliano) na Ibrahim Samuel ( Mkurugenzi wa Idara ya Masoko)
STARS YAANZA VIBAYA AFCON,YATANDIKWA 3-0 NA MOROCCO
TAIFA Stars imeanza vibaya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) baada ya kutandikwa mabao 3-0 na Morocco katika mchezo wa Kundi F uliopigwa usiku huu Uwanja wa Uwanja wa Laurent Pokou Jijini San-Pedro, Ivory Coast.
Katika mechi hiyo Stars ilimaliza pungufu baada ya kiungo wa Novatus Dismas Miroshi kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 70 kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya njano.
Morocco ilijipatia mabao yake kupitia na beki Romain Ghanem Paul Saïss , kiungo Marseille Azzedine Ounahi na mshambuliaji na Youssef En-Nesyri.
MEXIME AWAPIGA MKWARA WACHEZAJI WAKE
Kocha Mkuu wa Ihefu FC, Mecky Maxime amewataka wachezaji wake kutumia vipaji vyao ipasavyo ili kuipa matokeo mazuri timu hiyo.
Maxime alisema nafasi waliyopo kwenye msimamo haiendani na ukubwa wa majina na umaarufu waliokuwa nao wachezaji wake
“Ligi ya msimu huu ni ngumu inahitaji wachezaji wanaopambana na siyo umaarufu au ukubwa wa majina mimi na vijana wangu tunapaswa kupambana na kila mmoja kutimiza wajibu wake ili kuiondoa timu kwenye nafasi mbaya iliyopo hivi sasa,” alisema Maxime.
Aliongeza kuwa usajili walioufanya kwenye dirisha dogo ni mzuri na unakwenda kuwaongezea nguvu lakini kitu cha kwanza lazima kila mtu atimize jukumu lake la msingi.
Aliongeza kuwa na wachezaji wazuri wazuri siyo kitu muhimu sana kama wachezaji hao hawajitumi hivyo atahakikisha anaanda mpango mkakati maalumu utakaomwezesha kila mchezaji kuchangia mafanikio waliyoyakusudia.
Ihefu iliyopo nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi Kuu imefanya usajili mkubwa kwenye dirisha dogo baadhi ya wachezaji iliyo wasajili ni Elvis Rupia, Duke Abuya na Bruno Gomes wote kutoka Singida Fountain Gate
GAMONDI AMTABIRIA MAKUBWA GUEDE
KOCHA MKuu wa Yanga, Miguel Gamondi amemtabiria makubwa mshambuliaji mpya wa timu hiyo Joseph Guede akisema atawasaidia sana kutetea mataji yote ya ndani.
Yanga ilifunga dirisha dogo la usajili juzi kwa kumtambulisha Guede raia wa Ivory Coast kama mrithi wa Hafidh Konkoni ambaye kiwango chake hakikumvutia kocha huyo raia wa Argentina.
Gamondi alisema kupata saini ya mshambuliaji huyo ni sawa na kumaliza tatizo sugu la umaliziaji ambalo limemsumbua tangu aichukue timu hiyo mwanzoni mwa msimu huu.
“Naujua vizuri uwezo wa Guede, ni mshambuliaji aliyekamilika anajua kufunga lakini hata kutengeneza nafasi kwa wenzake binafsi imani yangu nikubwa kwake kitu cha msingi kwake ni kuthibitisha hilo kwa kufunga mabao yakutosha,” alisema Gamondi.
Licha ya uzoefu mkubwa aliokuwa nao kutokana na kucheza ligi mbalimbali Afrika na Ulaya,Gamondi amemtaka mchezaji huyo kupambana uwanja wa mazoezi ili kugombea nafasi ya kucheza na washambuliaji waliopo.
Alisema yeye ni kocha anayetenda haki hivyo pamoja na rekodi nzuri alizokuwa nazo kama atashindwa kujituma atamweka nje na kuwapa nafasi wachezaji wengine ambao watakuwa wanafanya vizuri mazoezini.
Guede ( 29),amejiunga na Yanga kwa mkataba wa miezi sita akitokea timu ya Tuzlaspor FC ya Uturuki.
TANZANIA YAJIFUNZA MAANDALIZI YA AFCON 2027 KUTOKA IVORY COAST
Na Brown Jonas – WUSM, Ivory Coast
WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Damas Ndumbaro ametembelea Uwanja wa Mpira wa Miguu wa Laurent Pokou uliopo jijini San Pedro nchini Ivory Coast ili kujifunza na kuona namna ambavyo nchi hiyo imefanya maandalizi ya uenyeji wa AFCON 2023 ikiwemo ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya mashindano hayo makubwa Afrika.
Dkt.Ndumbaro amefanya ziara hiyo sanjari na kuhudhuria mashindano ya Kombe la Mataifa Afrika (Afcon2023) yanayoendelea nchini humo kama sehemu ya Tanzania kuendelea kujiandaa na uenyeji wa mashindano hayo mwaka 2027 kwa kushirikiana na Kenya na Uganda.
Dkt. Ndumbaro amesema aina ya uwanja aliouona unafaa pia katika mikoa mbalimbali ya Tanzania ambapo amesema Serikali mbali na kuendelea kujenga viwanja vya michezo Dodoma na Arusha inaendelea kukaribisha wadau wengine kuunga mkono juhudi hizo katika ujenzi wa miundombinu ya michezo katika mikoa mingine.
Katika ziara hiyo,Dkt. Ndumbaro ameambatana na Kaimu Balozi wa Kituo cha Abuja anayehudumia pia nchi ya Ivory Coast, Judika Nagunwa, Kaimu Mkurugenzi wa maendeleo ya michezo Ally Mayay na maafisa wengine wa wizara.
MWAKINYO ACHAGIZA MAPRO
BONDIA Hassan Mwakinyo amesema mapromota wanaotaka kumewekea gari kwa ajili ya pambano milango iko wazi.
Mwakinyo aliandika ujumbe huo jana kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii akisema sasa yuko tayari kwa mapromota wanaotaka kumewekea gari kwa ajili ya kupigana kama zawadi.
“Haya sasa mapromota anayetaka kuniwekea gari milango iko wazi,”ulisomeka ujumbe huo huku akiwa ameweka picha ya gari kuonesha umuhimu wake.
Haitakuwa mara ya kwanza hapa nchini kwa bondia kupigana kwa ushindi wa gari kwani bondia kutoka Morogoro Twaha Kassim ‘Kiduku’ aliwahi kupigana na kushinda gari aina ya Toyota Crown mwaka juzi.
Mwakinyo kwa sasa anajiandaa na pambano la usiku wa Mtata Mtatuzi litakalopigwa Januari 27 mwaka huu kwenye Uwanja wa New Amaan Zanzibar dhidi ya bondia kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mbiya Kanku kuwania mkanda wa dunia wa WBO.
LOMALISA 'AJIFUNGA' MMOJA TENA YANGA
BEKI wa kushoto wa Yanga, Joyce Lomalisa ameongeza mkataba wa mwaka mmoja kuendelea kuitumikia timu hiyo.
Mkataba wa awali wa beki huyo unamalizika mwishoni mwa msimu huu hivyo uongozi kwa kushirikiana na benchi la ufundi umeamua kumuongeza mwaka mmoja kutoka na kuvutiwa na huduma yake.
Lomalisa alisema kilichomfanya kukubali kuongeza mkataba mpya ni malengo waliyokuwa nayo viongozi wa timu hiyo hasa katika mashindano ya kimataifa.
“Yanga ni sehemu salama kwangu viongozi wake wana maono ya mbali ndiomaana nimechagua kubaki hapa naamini nitafika mbali zaidi hasa katika mashindano ya kimataifa,” alisema Lomalisa.
Beki huyo alisema katika kipindi cha misimu miwili ambacho ameichezea timu hiyo amebaini mambo mengu mazuri ikiwemo kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kufika fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika msimu uliopita na kubeba ubingwa wa Ligi Kuu na Kombe la FA.
Alisema kwa sasa akili na mawazo yake ameyaweka kwenye klabu hiyo kuhakikisha anashirikiana na wenzake ili kuipa mafanikio zaidi katika mashindano yote ambayo wanashiriki msimu huu.
Lomalisa alijiunga na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili mwanzoni mwa msimu huu akitokea Petro Atletico ya Angola na tangu ajiunge amekuwa na mchango mkubwa kwenye kikosi cha kocha
TFF YAMPUMZISHA AMROUCHE,MOROCCO NA MGUNDA WAKABIDHIWA TIMU
STSRS,ZAMBIA ZAGAWANA POINTI AFCON
TIMU ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' leo imelazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya Zambia katika mchezo wa Kundi F kwenye michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON).
Stars ilitangulia kupata bao hiko kupitia shuti kali la Simon Msuva katika dakika ya 11 bao ambalo lilizipeleka mapumziko timu hizo kwa Stars kuingoza 1-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa kila timu kucheza kwa tahadhari kubwa kabla ya Patson Daka kusawazisha katika 88 kwa mpira wa kichwa.
Kwa matokeo hayo yanaifanya Tanzaia kuendelea kushika mkia katika kundi F kwa kuwa na pointi moja ambapo Morocco inaongoza ikiwa na pointi 4, ikifuatiwa Zambia (2) na DR Congo (2).
Michezo iliyosalia itapigwa keshokutwa Jumatano Januari 24, 2024 ambapo Tanzania itakipiga na DR Congo na Zambia itakwaana na Morocco